Translate

Tuesday, August 4, 2015

Faida ya Tunda la parachichi mwilini (AVOCADO)



FAIDA YA TUNDA LA PARACHICHI - PEA (AVOCADO)
Ndani ya tunda hili kuna maji kiasi kidogo sana ukilinganisha na matunda mengine lakini kuna mafuta mengi na unaweza kuchanganya kula na tunda lingine kama vile apple, ndizi, chungwa au hata maziwa kwa kutengeneza juisi.

TINDIKALI
Licha ya kuwa na mafuta parachichi lina tindikali (acid) mbalimbali ikiwemo inayojulikana kama amino ambayo husaidia sana kukinga na kutibu maradhi katika mwili wa binadamu. Tunda hili pia lina protini ya kiwango cha juu.
Pia kuna tindikali inayoitwa oleic acid kwenye parachichi ambayo husaidia kukinga magonjwa ya moyo, kiharusi na kansa.

VITAMINI “E” NA B6
Imeelezwa na wataalamu kuwa tunda hili lina kiwango kikubwa cha vitamini E kuliko ile inayopatikana kutoka kwenye mazao ya wanyama.Parachichi lina vitamini hiyo nyingi kuliko inayopatikana katika mayai ambayo yanasifika kwa kuwa na vitamini e, hivyo hii inathibitisha kuwa lina faida kubwa mwilini.

Yemen yakabiliana na waasi wa Houthi



Wanajeshi wa serikali wameanzisha mashambulio makali yenye lengo la kuwafurusha waasi wa Kihouthi kutoka eneo moja lililokuwa kituo cha wanajeshi wa anga huko mjini Aden.
Kuna ripoti kuwa waasi kadhaa waliuawa .
Kituo hicho muhimu kiitwacho Al Anad kilikuwa pia kikitumiwa na majeshi ya Marekani waliokuwa wakitumia ndege zisizo na rubani kuwalenga wanachama wa kundi la Al Qaeda walioko Yemen.

Mawaziri watano waanguka kura za maoni


Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kiislamu

Kwa ufupi

  • Ni Chikawe, Makalla, Silima, Ole Telele na Mahadhi
  • Pia yumo Katibu wa NEC CCM Muhamed Seif Khatib
  • Profesa Muhongo, Muradi, Mwakalebela, Nape wapita
Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kiislamu Kondoa Dodoma, Hamisi Salum akikabidhi kadi ya CCM kwa ajili ya uhakiki wa taarifa zake kabla ya kupiga kura kumchagua mgombea udiwani na ubunge wa jimbo hilo katika Kituo cha Maji ya Shamba. Awali, kura za kituo hicho zilichomwa baada ya kubainika kuwa na udanganyifu. Picha na Shakila Nyerere .

Friday, July 10, 2015

Nani msafi wa rushwa ndani ya ccm?


pic+vichwa

Vikao vya maamuzi ya CCM vimeanza Dodoma. Huku wanachama na wapenzi wa CCM Macho na masikio yao yakiwa yametegeshwa dodoma kusubiri ni nani atakayeteuliwa kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Kwa miaka yote ambayo CCM imeshirki chaguzi kama hizi huko nyuma, Ni mwaka huu pekee ambapo CCM imekuwa katika wakati mgumu.

Thursday, April 30, 2015

Rais KIKWETE afanya mazungumzo na BILL CLINTON


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha na kisha kufanya mazungumzo na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe Bill Clinton Ikulu jijini Dar es salaam
Rais JAKAYA KIKWETE amekutana na kufanya mazungumzo ya faragha na Rais wa 42 wa MAREKANI - BILL CLINTON ambaye anaendelea na ziara yake nchini. 

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais IKULU Jijini DSM imesema kuwa wakati wa mazungumzo yao viongozi hao wamezungumzia baadhi ya miradi inayodhaminiwa na kugharimiwa na Taasisi ya CLINTON. 

Miradi hiyo ni ile iliyopo katika sekta ya afya na hasa katika utoaji wa dawa za kurefusha maisha kwa watu wanaoishi na virusi vinavyosababisha ukimwi, afya za akina mama na jinsi ya kupunguza vifo vya watoto walio na umri wa chini ya miaka mitano.